• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Maliasili, Ardhi na Mazingira

  • MPANGO KAZI WA MRADI WA USIMAMIZI WA MALIASILI KWA AJILI YA MAENDELEO YA WANANCHI KIUCHUMI (NRM LED), WILAYA YA KAKONKO

KAZI ZILIZOFANYIKA KWA ROBO YA PILI YA MWAKA 2016/2017.

 

Tokeo tarajiwa 1:

Kujenga uwezo kwa Serikali za Mitaa juu ya kuweka Vipaumbele vya Maliasili katika Mipango ya Bajeti kuanzia ngazi ya Kijiji hadi Wilaya.

Kujenga uwezo kwa timu ya uwezeshaji ya wilaya jinsi ya mtiririko wa utoaji wa taarifa 

 

Tokeo tarajiwa 2:

Kuboresha utawala bora na usimamizi endelevu wa maliasili kupitia kamati za usimamizi za vijiji na watumiaji wakuu wa rasilimali hizo katika ngazi ya kijiji

Kujenga uwezo na utekelezaji wa mpango wa matumizi bora ya ardhi ya vijiji kwa kuboresha utawala bora na usimamizi endelevu wa maliasili ikiwa ni pamoja na kuwezesha mpango wa matumizi bora ya ardhi wa vijiji

Kuunda kamati ya matumizi bora ya ardhi katika kila kijiji (VLUM), katika vijiji vya Rumashi, Nyabibuye, Churazo, Gwarama na Kabare

Kutoa mafunzo kwa kamati ya matumizi bora ya ardhi juu ya hatua za kufuata wakati wa kuandaa matumizi bora ya ardhi, katika vijiji vya Rumashi, Nyabibuye, Churazo, Gwarama na Kabare

Kufanya utambuzi wa mipaka ya vijiji/kujua mipaka ya kijiji chao ,eneo la ardhi yao ya kijiji  na kujua matumizi ya ardhi yao  kwa sasa, katika vijiji vya Rumashi, Nyabibuye, na Churazo

Kuijengea uwezo timu ya wawezeshaji wa Mpango shirikishi wa jamii wa msitu (PFM) juu ya hatua sita za kuandaa mpango shirikishi jamii wa msitu

Kuhuisha/kuunda kamati za Maliasili za vijiji katika vijiji vya Rumashi, Nyabibuye, Churazo, Gwarama na Kabare

Kufanya mafunzo kwa kamati za Maliasili juu ya majukumu na wajibu, Sera na Sheria zinazohusiana na Maliasili, katika vijiji vya Rumashi, Nyabibuye, Churazo, Gwarama na Kabare

Tokeo tarajiwa 3:

Watumiaji wakuu wa maliasili,wachakataji wa mazao ya maliasili,na wafanayabaishara wa maliasili wafanye shughuli  za maliasili kwa faida na kwa uendelevu

Kutambua na kuainisha vikundi vya kuweka na kukopa na vikundi vya kijamii vilivyopo katika maeneo ya mradi, katika vijiji vya Rumashi, Nyabibuye, Churazo, Gwarama na Kabare

Kufanya ziara za kuwajengea uwezo/mfunzo VICOBA,SACCOS na vikundi vya kijamii, vijiji vya Kazilamihunda na Juhudi

 

Tokeo tarajiwa 4:

Kuimarisha uwezo wa kitaasisi na uwajibikaji wa wadau muhimu kwa ajili ya kuboresha ushiriki wa jinsia,utawala bora, uratibu wa Ukanda (landscape), na utekelezaji wa usimamizi shirikishi wa maliasili

Kutambulisha mradi katika ngazi ya kijiji (mkutano wa hadhara) na ngazi ya kata (Baraza la maendeleo la kata-WDC), katika vijiji vya Rumashi, Nyabibuye, Churazo, Gwarama na Kabare

Kuanzisha na kuziwezesha klabu za mazingira kwenye shule za msingi (7) na sekondari (3,) katika vijiji vya Rumashi, Nyabibuye, Churazo, Gwarama, Kabare, Kazilamihunda na Juhudi

Wafanyakazi wa Halmashauri kwa kushirikiana na wananchi wa kata ya walipanda miti kwenye vyanzo vya mbizi na Kabare siku ya kupanda miti kitaifa ili kutunza vyanzo vyetu vya maji.

Watendaji wa kata na watendaji wa Vijiji walihimizwa kusimamia zoezi la upandaji miti kwenye vyanzo vya maji katika maeneo yao ili kuweza kulinda na kutunza mazingira na vyanzo vyetu vya maji.

Tumeweza kuwadhibiti na kupambana na wanyama waharibifu katika vijiji vinavyozunguka hifadhi ya moyowosi.

 

 

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA KIPINDI CHA ROBO YA PILI YA MWAKA 2016/2017 KITENGO YA ARDHI KAKONKO

           1.1 Utangulizi

Idara ya Ardhi Wilayani Kakonko inatekeleza majukumu yake kulingana na Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995, Sera ya Maendeleo ya Makazi ya mwaka 2000, Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999, Sheria ya Ardhi ya Vijiji Na. 5 ya mwaka 1999, Sheria ya Upimaji na Ramani ya mwaka 1957 na Sheria ya Mipangomiji Na. 8 ya mwaka 2007. Sheria hizo zinatekelezwa sambamba na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Na. 7 ya mwaka 1982 na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Na. 8 ya mwaka 1982 na Kanuni za Upangaji Viwango vya Upimaji Mjini za mwaka 2011.

Ifuatayo sasa ni taarifa fupi ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya Kitengo cha   Ardhi kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2016/2017.

1.2 Upimaji wa viwanja.

Kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2016/2017 Kitengo cha Ardhi kimefanikiwa kupima viwanja vifuatavyo:

Viwanja 125 ambavyo vimewekwa alama na majira nukta (Dermacation na coordination) kazi ya kupanda mawe ya upimaji(beacons) inaendelea kwa maeneo yasiyokuwa na marekebisho ya kitaalam ili kuweza kuchora ramani ya Upimaji (Survey Plan) kwa ajili ya kupeleka Wizara ya Ardhi kuidhinishwa na mkurugenzi wa Upimaji na Ramani.

 1.3 Uandaaji wa Hatimilki.

Kitengo cha Ardhi kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2016/2017 kimezidi kuandaa hati kwa wananchi na kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kuwa na hati miliki.

 1.4 Ukaguzi wa ujenzi.

Katika kipindi cha robo ya pili iliyopita, kitengo cha Ardhi kimefanya ukaguzi katika maeneo ya Kakonko Mjini kwa ajili ya kudhibiti ujenzi holela katika maeneo hayo. Aidha katika kipindi hicho, wadau mbalimbali wa ujenzi walihamasishwa kuwasilisha ramani za nyumba walizotazamia kujenga ili wapatiwe vibali vya ujenzi. Hii ni katika kutekeleza Sheria ya Mipangomiji namba 8 ya mwaka 2007 kifungu cha 29 ambacho kinazuia maendelezo yoyote ya ardhi kufanywa bila kuwa na idhini na kibali cha ujenzi.

1.5 Migogoro ya Ardhi.

Migogoro ya ardhi imekua ikitokea baina ya mtu na mtu, kijiji na kijiji, migogoro baina ya mtu na mtu ofisi ya ardhi imekua ikijaribu kutoa ushauri wa kitaalam ili kuleta maridhiano baina ya pande mbili,

Pia migogoro ya Kijiji na Kijiji imekua ikiibuka kwa vijiji ambavyo vimegawanyika na kuzaa vijiji vipya,Mfano uliokuwa  Mgogoro wa Kijiji cha Kabare na Luhuru, ufumbuzi wa mgogoro huo ni kutokana na sharia ya Ardhi No 4 na No 5 ya mwaka 1999 kila raia anahaki ya kufanya shughuli popote ndani ya nchi ya Tanzania,kwahiyo basi Mgogoro huu suluhisho lake limepatikana  kwa Vijiji vyote viwili kuridhia mpaka wa kutenganisha vijiji hivyo bila kuadhiri shughuri zate zilizokuwa zinafanywa kwa pande zote mbili  na utaratibu wa kuvipima vijiji hivyo utafuata kwa kushirikisha pande zote mbili.

Mgogoro wa mashamba kati ya wananchi wa Kijiji cha Kiga na Nyakayenzi nao suluhu imepatikana kwa kutumia ibara ya 24(1) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na bila kuathiri vifungu vifungu vingine vya sheria za ardhi kila mtu anaruhusiwa na anayo haki ya ulinzi wa mali yake kwa mujibu wa sheria.

Ardhi yote ya Tanzania ni mali ya Umma (kwa mujibu wa sheria ya ardhi namba 4 na sheria ya ardhi ya Vijiji namba 5 ya mwaka 1999) kila Mtanzania anayo haki ya kumiliki na kutumia ardhi popote pale ndani ya mipaka ya Tanzania kwa mujibu wa sheria, kwahiyo basi kila mwananchi aliyekuwa akimiliki na kulima mashamba kwenye bonde la mto Ruhwiti kabla ya mipaka ya vijiji vya Nyakayenzi na Kiga kuwekwa, ataendelea kumiliki na kulima katika eneo hilo bila kujali eneo hilo lipo katika Ardhi ya kijiji cha Nyakayenzi au Kiga. Kwa maana hiyo Wananchi wa Kijiji cha Kiga waliokuwa wanamiliki na kulima mashamba katika eneo la mto Ruhwiti kabla ya mipaka kuwekwa wataendelea kulima katika eneo hilo. Aidha Kijiji chochote kinachohitaji kurejeshewa maeneo/ Ardhi hiyo inayomilikiwa na kutumiwa na wananchi wa kijiji kingine wanajibika kufuata taratibu na sharia za kurejeshewa maeneo / Ardhi yao ikiwa ni pamoja na kulipa fidia wale wote waliokuwa wanamiliki mashamba kwenye maeneo hayo baada ya wataalam kutoka ngazi ya halmashauri kutathmini maeneo hayo na si vinginevyo.

Hivyo basi ni wajibu wa kila Halmashauri ya Kijiji husika na wananchi wake kuzingatia maamuzi na makubaliano yaliyofikiwa ili shughuli zote za maendeleo ziweze kufanyika pasi kuendeleza migogoro isiyo na tija.

Matangazo

  • FORM I 2021 JOIN INSTRUCTIONS December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Ujenzi wa stendi ya kisasa Kakonko waanza kutekelezwa kwa gharama ya Tsh.2.1 bilioni kwa siku 365

    June 20, 2019
  • Hospitali ya Wilaya ya Kakonko yapokea msaada wa vifaa tiba na madawa ya Tsh.88,295,430/=

    May 02, 2019
  • BALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA AKABIDHI VIFAA VYA MIFUGO KAKONKO

    January 24, 2019
  • MIRADI 3 YA MAJI YA BILIONI 1.5 KUTEKELEZWA NDANI YA MIEZI 6 KAKONKO

    June 08, 2018
  • Tazama zote

Video

Maadhimisho ya siku ya wanawake kitaifa yafanyika kwa ufanisi Mkoani Simiyu Machi 8, 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Pakua hati yako ya malipo ya mshahara Hapa "Utumishi Portal"
  • Tangazo la zabuni
  • Matokeo ya Mitihani ya baraza
  • Nafasi za kazi zinazotolewa na Sekretalieti ya Ajira
  • Taarifa kwa Umma zinazotolewa na "TAMISEMI"

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: 028-2820137

    Simu ya Mkononi: 0757470800

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa