• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

MIRADI 3 YA MAJI YA BILIONI 1.5 KUTEKELEZWA NDANI YA MIEZI 6 KAKONKO

Imetumwa: June 8th, 2018


Mikataba 3 ya Miradi ya maji yenye thamani ya bilioni 1,573,000,000 imesainiwa na kupangwa kutekelezwa katika kipindi cha miezi 6 Wilayani Kakonko. 

Kaimu mhandisi wa maji, Matwiga Victor Tandali ameeleza hayo katika hafla ya kusaini mikataba hiyo iliyofanyika hivi karibuni katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ambapo wakandarasi watatu wamesaini mikataba.

 Mradi wa kwanza utakuwa ni ujenzi wa mradi wa maji Kakonko utakaogharimu milioni 299.6 na kutekelezwa na kampuni ya Santiago. Mradi huo unatokana na fedha za matokeo ya haraka (Quickwins) ambapo mradi utajikita katika kuchimba visima na kupanua mtandao na kufikisha maji makao makuu ya Halmashauri na maeneo ya jamii.

Bwana Matwiga ameongeza kuwa mradi wa pili utahusika katika kuweka nishati ya jua katika kata ya Gwanumpu na kugharimu milioni 623.2 na kutekelezwa na kampuni ya MS Gross.

Aidha mradi wa tatu utafanyika katika kata ya Nyabibuye ukilenga kufanya ukarabati mkubwa na kupanua maeneo ya huduma ya mradi ambao ni wa kutega unaogharimu milioni 660.2 na kutekelezwa na kampuni ya OBD.

Mhandisi wa maji ameongeza kuwa lengo ni kuhakikisha wanatekeleza majukumu ya sekta ya maji kimkakati kwa kuangalia dira ya mwaka 2025 na ilani ya uchaguzi.

Diwani wa kata ya Nyabibuye ambaye ni mnufaika wa mradi, Stephen Munigankiko ameeleza kuwa wakazi wa Kijiji cha Nyabibuye walikuwa hawapati huduma ya maji hivyo mradi ukikamilika utakuwa ni msaada na mkombozi mkubwa kwao.

Mmoja wa mkandarasi aliyepata kazi, Santiago ameeleza kuwa wapo tayari kufanya kazi kwa moyo wanachohitaji ni kupata ushirikiano kutoka kwa viongozi. Hata hivyo aliwaomba wanasiasa kufanya kazi zao za kisiasa na kutoa nafasi kwa wakandarasi kufanya kazi zao za kitaalam.

Kwa mujibu wa mhandisi Matwiga kwa sasa miradi ya maji inayotekelezwa Kakonko mjini imefikia hatua 45% lakini miradi itakapokamiika itafikia asilimia 65% wakati kwa upande wa vijijini ni 50% kwa sasa na inategemewa kufikia 58% miradi itakapokamilika.

Wadau wa maendeleo wakiwemo Water Mission wamefadhili mradi wa maji wa Kakonko mjini kwa kuchimba visima nakuweka nishati ya jua mabapo mradi umegharimu milioni 222. 

Matangazo

  • FORM I 2021 JOIN INSTRUCTIONS December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Ujenzi wa stendi ya kisasa Kakonko waanza kutekelezwa kwa gharama ya Tsh.2.1 bilioni kwa siku 365

    June 20, 2019
  • Hospitali ya Wilaya ya Kakonko yapokea msaada wa vifaa tiba na madawa ya Tsh.88,295,430/=

    May 02, 2019
  • BALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA AKABIDHI VIFAA VYA MIFUGO KAKONKO

    January 24, 2019
  • MIRADI 3 YA MAJI YA BILIONI 1.5 KUTEKELEZWA NDANI YA MIEZI 6 KAKONKO

    June 08, 2018
  • Tazama zote

Video

Maadhimisho ya siku ya wanawake kitaifa yafanyika kwa ufanisi Mkoani Simiyu Machi 8, 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Pakua hati yako ya malipo ya mshahara Hapa "Utumishi Portal"
  • Tangazo la zabuni
  • Matokeo ya Mitihani ya baraza
  • Nafasi za kazi zinazotolewa na Sekretalieti ya Ajira
  • Taarifa kwa Umma zinazotolewa na "TAMISEMI"

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: 028-2820137

    Simu ya Mkononi: 0757470800

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa